Mwnamuziki nyota na mkongwe mwenye asili ya Congo King Blaise Mfalme wa band ya Fm Academia amewashangaza watu wa media hasa watangazaji baada ya kuachia wimbo wa dansi wenye dakika tano tu alafu mzuri sana

Wimbo huo uitwao DADA HUYO ukiwa ni utunzi wake kupitia band yake ya fm academia umekuwa gumzo kutokana na uzuri wa wimbo na uchache wa dakika kitu ambacho kimewashangaza watangazaji wengi wa vyombo mbali mbali vya habari kwani walishazowea nyimboza dansi nilazima ziwe na dakika nyingi

Wengi tunafahamu kuwa mara nyingi nyimbo za dansi zimekuwa na kawaida ya kuwa ndefu kuanzia dakika nane hadi kumi na zaidi ,lakini kwa sasa mambo yameanza kubadilika kwa nyimbo za dansi kufupishwa 

Hilo limejidhihirisha kupitia wimbo huu wa DADA HUYO utunzi wa king Blaise 

Zipo band ambazo zimejaribu kutoa nyimbo zenye dakika chache lakini hazikuweza kuwa gumzo au kuonyesha dalili ya kupendwa na kushtua watangazaji kama wimbo huu wa dada huyo ambao upo hewani kwa sasa

Baadhi ya watangazaji waliyosikia wimbo huu na kucheza radioni walishtuka na kusema kuwa kumbe inawezekana wimbo wa dansi kuwa mfupi na ukawa mzuri (kama kushtuka na kushangaa)

Lakini kwa upande wake mtunzi wa wimbo huu King blaise amesema alitunga wimbo huu muda mrefu na kama angerekodi kadiri ya alivyo utunga basi ungekuwa na dakika kumi au kumi na mbili 

“unajua wimbo nimetunga zamani sana na kama ningerekodi kama nilivyo utunga ungekuwa na zaidi ya dakika kumi au kumi na mbili ,lakini sasa mambo yanabadilika kwa hiyo mimi kama mwanamuziki lazima nisome alama za nyakati kwa kujua soko la muziki sasalipovipi na mashabiki wanataka nini kwa wakati gani”

Nao Baadhi ya mashabiki wa dansi kupitia mitandao ya kijamii wamesema kuwa wameshawahi kusikia nyimbo za dansi zenye dakika chache lakini hazina kiwango kama wimbo huu wa DADA HUYO

Wimbo wa DADA HUYO umetungwa na King Blaise umerekodiwa katika ya alain mapigo lakini waliyotia rap ni Gseven na Bodack Nduala Mp3 huku gitaa la solo likicharazwa na mkongwe Christian mene Mukambilwa 
 
Wimbo huu kwa sasa upo katika mitandao ya kijamii ikiwemo you tube ila official video is coming soon

TAZAMA SIMPLE VIDEO HAPA CHINI

AddThis

 
Top