MABINGWA wa Kandanda Tanzania bara, Young Africans leo wanaendelea kujifua uwanja wa Karume, Dar es salaam ikiwa ni siku ya tatu mfululizo tangu waanze maandalizi ya kujiwinda na ligi kuu msimu ujao, kombe la Kagame na michuano ya klabu bingwa barani Afrika.
Yanga imekuwa timu iliyoanza mazoezi mapema ikilinganishwa na timu nyingine za Dar es Salaam ambazo ni Simba na Azam fc.
Kocha mkuu wa Yanga Hans van der Pluijm akiwa kazini
Kocha  mkuu wa  klabu hiyo, Mholanzi, Hans van der Pluijm amesema wataendelea kufanya mazoezi katika Uwanja wa Karume wakati huu wanawasubiri wachezaji wote waliopo timu za taifa  za nchi zao yaani Taanzania, Rwanda na Burundi.

"Ukianza mapema, unakuwa na nafasi ya kuamua mambo mengi, ubadili nini au uongeze kipi. Kuanza mapema pia kunasaidia wachezaji kuwa fiti zaidi," amesema Pluijm.

AddThis

 
Top