Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaendelea kujinoa katika uwanja wa  Addis Ababa zamani ukifahamika kama Haille Sellsie uliopo jijini Addis Ababa kujiandaa na mchezo dhidi ya Misri kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika 2017 utakaopigwa Juni 14, jijini Alexandria.
Afisa.
Afisa habari wa Shirikisho la soka nchini TFF aliyeambatana na timu hiyo huko Ethiopia, Baraka Kizuguto amesema kikosi cha Stars kinakwea pipa kesho jioni kuwafuata Mafarao wa Misri.
“Timu inatarajia kuondoka kesho Ijumaa jioni kuelekea Cairo, kwasasa bado timu inaendelea kufanya mazoezi hapa Addid Ababa katika uwanja wa Taifa”. Amesema Kizuguto na kufafanua: “Leo jioni timu inafanya mazoezi katika uwanja wa Taifa (Ethiopia) hali kadhalika kesho, lakini mara baada ya mazoezi ya kesho kikosi kitasafiri kwenda Cairo, kikifika kitaunganisha moja kwa moja kwenda Alexandria Jumamosi asubuhi kujiandaa na mechi itakayochezwa jumapili”.

AddThis

 
Top