Wanandinga Mohamed Hussein 'Tshabalala' (Simba), Mrisho Ngassa (Yanga) na
Simon Msuva (Yanga) wanachuana kuwania tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu Tanzania
bara msimu wa 2014/20145 iliyoandaliwa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kwa
kushirikiana na wadhamini wa Ligi Kuu kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.
Kwa upande wa makocha, Goran Kopunovic (Simba), Hans vand
der Pluijm (Yanga) na Mbwana Makata (Prisons) wanachuana kuwania tuzo ya kocha
bora wa VPL.
Hafla ya utaoaji wa zawadi kwa washindi wa Vodacom Premier
League (VPL) msimu wa 2014/2015 inatarajia kufanyika leo katika katika ukumbi
wa JB Belmonte (Kilimanjaro) uliopo katika jengo la Golden Jubilee Tower
(PSPF), mtaa wa Ohio eneo la Posta Mpya, jijini Dar es salaam kuanzia saa 12 jioni.
Mgeni rasmi katika halfa hiyo ya utoaji zawadi kwa wachezaji,
makocha, na timu washindi atakua ni Juma Nkamia, Naibu Waziri wa Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo.
Vodacom watatoa zawadi kwa Bingwa wa Ligi Kuu msimu
2014/2015, mshindi wa pili, mshindi wa tatu na mshindi wa nne, baadhi ya
vipengele vitakavyotolewa zawadi pia na wadhamini hao wa Ligi Kuu ni :
1. Mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom 2014/2015
Mohamed
Hussein (Simba SC)
Mrisho Ngasa
(Young Africans)
Saimon Msuva
(Young Africans)
2. Mlinda mlango bora wa Ligi Kuu ya Vodacom 2014/2015
Mohamed Yusuph
(Tanzania Prisons)
Said Mohamed
(Mtibwa Sugar)
Shaban Hassan
(Coastal union)
3. Kocha bora wa Ligi Kuu ya Vodacom 2014/2015
Goran Kopunovic
(Simba SC)
Hans Van Der
Pluijm (Young Africans)
Mbwana Makata
- (Tanzania Prisons)
4. Mwamuzi bora wa Ligi Kuu ya Vodacom 2014/2015
Israel Mjuni Nkongo
Jonesia
Rukyaa
Samwel Mpenzu
5. Timu yenye nidhamu Ligi Kuu ya Vodacom 2014/2015
Mgambo JKT
Mtibwa Sugar
Simba SC